Wakati leo dunia ikiadhimisha siku ya Mazingira, Wananchi wameaswa kuungana na kuhifadhi mazingira kwa manufaa ya vizazi vya sasa na vijavyo Na Hagai Ruyagila Wananchi Wilayani Kasulu Mkoani Kigoma wametakiwa kutumia nishati safi ya kupikia ili kutunza na kuhifadhi mazingira na kuepukana na changamoto ya ukataji wa miti ambayo inatajwa kuwa chanzo cha mabadiliko ya tabia nchi.