Kumekuwa na makabiliano makali kati ya wajumbe wa Urusi na Marekani katika Baraza la Usalama la Umoja wa Mataifa, baada ya Marekani kuitisha mkutano wa kujadili kuhusu upelekwaji wa wanajeshi wa Urusi kwenye mipaka yake na Ukraine.
Balozi wa Marekani Linda Thomas-Greenfield alisema upelekwaji huo ulikuwa mkubwa zaidi Ulaya kuwahi kuonekana katika miongo kadhaa.
Mwenzake wa Urusi aliishutumu Marekani kwa kuchochea hali ya wasiwasi na uingiliaji usiokubalika katika masuala ya Urusi.