
Donald Trump amekana mashtaka 34 yanayohusiana na kughushi rekodi za biashara, kutokana na malipo ya kimyakimya yaliyotolewa kwa nyota wa filamu ya utupu Stormy Daniels mnamo 2016.
Aliondoka nyumbani kwake huko Trump Tower muda mfupi baada ya 13:00 saa za ndani (18:00 BST). Alipungia kamera zilizomsubiri akikunja ngumi, kabla ya kuingia kwenye gari lake.

Ilichukua dakika chache kwa msafara wa rais huyo wa zamani kusafiri umbali wa kilomita 6.4 (maili 4) kwa gari kutoka nyumbani kwake huko Trump Tower hadi Mahakama ya Jinai ya Manhattan. Wakati wa safari hiyo, alichapisha kwenye mtandao wa kijamii: “Inaonekana ajabu — WOW, watakuja KUNIKAMATA”.
Alionekana mtulivu alipokuwa akiingia ndani ya mahakama, akisimama kuupungia mkono umati.
