
Mabosi wa Etihad watakaa chini na mshambuliaji huyo mwenye mabao 42 mwishoni mwa msimu huu kujadili mkataba mpya wa pauni 500,000 kwa wiki.
Haaland yuko katika mwaka wa kwanza wa kandarasi ambayo itaendelea hadi 2027 na City wanapanga kuongeza hiyo kwa miezi 12. Wanataka kumtuza kwa mwaka wa kwanza mzuri England – na matumaini ya KO Real kumpeleka Mnorwe huyo, 22, kwenye LaLiga siku za usoni. Haaland kwa sasa anapokea mshahara wa wiki wa pauni 375,000 – kiwango cha juu zaidi cha Prem na mchezaji mwenzake Kevin De Bruyne na kipa wa Manchester United David de Gea – na vifungu vingine vya ziada. Hata hivyo wakala wake Rafaela Pimenta amechochea tetesi za kuhamia Madrid wakati fulani, akidai kuwa Real ni “ndoto” kwa wachezaji.